tangazo one

tangazo one

Abidal

Abidal

karibuni

ni mara chache sana tunapata muda wa kujiuliza juu ya umuhimu wa watu waliotuzunguka, na maisha yetu yangekuwaje bila wao? wape nafasi na usisite kuwaambia jinsi unavyojisikia juu yao na umuhimu wao kwako. ASANTE KWA KUWA SEHEMU YA MAISHA YANGU.

Wednesday, November 16, 2016

Pombe

Ebwana kuna jirani yangu amerudi amelewa sasa naskia anagonga mlango wake karibu masaa mawili hivi wakati hapa anaishi peke yake, sijui niende nikamwambie kuwa mwenyewe hayupo katoka?

Punguzeni pombe jamani

Maisha Magumu

Kweli maisha magumu kuna station ya tv ilisema Leo kipindi cha mapishi kitakuwa wali samaki...naona now wanaomba radhi eti watapika ugali na mchicha......

Saturday, October 1, 2016

Chizi

Chizi kakaa ukingoni mwa bahari analia kwa masikitiko na huku kakamata kijiko cha chai. Mwezake akamuuliza mbona unalia mwenzangu. Chizi akajibu nimetia vijiko vitatu vya sukari baharini, kila nikionja bado ina chumvi. Mwenzake akacheka sanaaaaaa akamwambia. Hujakoroga!!!!

Thursday, September 29, 2016

Nyoka

umerud geto mida ya saa mbil ucku unaingia ndan ghafla unamuona nyoka kanyanyua shngo juu ana chzesha mkia na ki ulimi kinatoka toka nje.....Kwa ujasili unaamua kuchukua fmbo ili kumuua ...lkn ulivo jasiri zaid unaamua kufnga na mlango af funguo unatupia ktndan unajarbu kumdhuru lkn ghafla umeme unakatika
Hapo ndo utajua nobody can stop Reggae

Wednesday, September 28, 2016

Daladala

Nimepanda daladala inavuja mpaka nikamshauri dereva aache kubeba abiria alime mchicha, hatuwezi kulowa hivi kwa daladala.

Sipendi uzembe mimi

Friday, September 23, 2016

Mwizi

Et jana usiku mwiz kavunja mlango kwangu
akaanza kutafuta kitu kila kona ikabid
na mie niamke namuuliza unatafuta nini ananijibu hela ndipo nilipoanza na mie kutafuta nae
maana hta hela ya kula Jana sikua
nayo alichoka zaid nilipomuliza una uhakika uliweka humu?
sipendagi utani na kitu hela mm!

Nani aliuwa Goliath

WAZAZI PELEKENI WATOTO SUNDAY SCHOOL PLEASE!!

TEACHER: Nani aliuwa Goliath......
STUDENT 1: Sio mimi.
STUDENT 2: Sikuwa shule jana. .
STUDENT 3: Mimi sijui.

(The Teacher went and told the Headmaster ati watoto wa hio class hawajui nani aliuwa Goliath.) ... ( headteacher goes to the class.)

HEADTEACHER: Nani aliuwa Goliath.
CLASS: Sio sisi.
H.TEACHER: Mkikosa kuniambia hii darasa itawaka moto.
CLASS: Hatujui teacher.

The H.TEACHER turns and asks the teacher....

"Uko sure Goliath aliuliwa na mtu wa hii
darasa?"

The teacher fainted...

Wednesday, September 21, 2016

Mke wangu

ETI NAMTONGOZA DEMU NAMPA NAMBA ALAFU ANAMPA BOYFRIEND WAKE AKANIPIGIA WE NANI UNAMTONGOZA MKE WANGU NIKAMJIBU MI MUHUDUMU WA GEST MWAMBIE AMESAHAU CHENCHI

Nimekunja sura

Leo kuna mtu nimemtolea uvivu ! amenikuta nimetulia akaniuliza mbona nimekunja sura ...nikamwambia nataka kuiweka kwenye bag.

Sipendangi ujinga mimi

Nilikula kuku

Unamualika binti luch harafu anakuja na maringo, eti oooh.....! Bebe ata sitakula wakati natoka home nilikula kuku....!!

Wewe kwa ugetlemen wako unamnunulia Whisky ya Jack Daniels ya elfu hamsini!

Baada ya binti wa watu kunywa mafunda kadhaa anatapika makande na mahindi ya kuchoma wallah...!!

Sasa apo inabidi umulize romantically .....!!

Sory baby...! Uko sure ulikula kuku au chakula cha kuku

Monday, September 19, 2016

Simu

Siku moja mfanyakazi alienda ofisini uku masikio
yake yote mawili yakiwa yamefungwa bandeji.
Bosi wake akamuuliza imekuaje kuhusu masikio
yako?. Jamaa akajibu.
"jana wakati napiga pasi nguo zangu, simu iliita, kwa
bahati mbaya badala ya kuweka simu sikioni nikaweka pasi".
"Sawa" Bosi akasema, "iyo ni kuhusu sikio moja, na
ilo sikio lingine ilikuaje?" Jamaa akajibu
"simu iliita tena!"

Wazazi wako

Unakutana na mdada ndani ya miezi miwili anataka aje waona wazazi wako. Dada, mi mwenyewe nlikaa miezi 9 tumboni kabla sijawaona wazazi wangu mwenyewe, usiniletee mapenzi ya Mwendokasi.

Sipendagi ujinga mimi

Nyumba za kupanga

UTAMU WA NYUMBA ZA KUPANGA!
Jana neighbor yangu alikuja
akaniambia nipunguze sauti ya radio
anataka kulala.
Leo anapika chapat na mimi
nmemwambia apunguze harufu ya
chapati nataka kula ugali. sipendi ujinga ajue.

Sunday, September 18, 2016

Vipofu

Jion ya jana niliwakuta  vipofu wawili wakipigana
Basi nikapaza sauti na kusema ninamsapoti huyo aliye na kisu
Ghafla wote wakaanza kukimbia mmoja kule mwingne huko.
Ila hakuna aliyekuwa na  kisu

Huwa sipendagi ugomvi mimi

Malaika

MTOTO: mama kwa nn unamuita mdogo angu malaika
MAMA: kwa sababu yeye ni mdogo sana na yupo kama malaika,
kwa nini umeuliza mwanangu?
MTOTO: nimemrusha dirishani nashangaa hajapaa

mama kazimia!!!

Friday, September 16, 2016

Mkopo

Kuna mdada nilimkopesha pesa kwa ahadi kuwa baada ya wiki moja atanirejeshea pesa zangu.

Baada ya wiki moja nampigia simu hapokei simu zangu, nimempigia zaidi ya mara kumi (10) bila ya mafanikio!

Kila nikimpigia simu hajibu simu zangu, nikahamua kumwandikia message kwa WhatsApp...!

Hello Mamu, Nakupigia simu sio kukudai pesa zangu, ila nataka kukwambia kuwa hapa Ubungo Plaza kuna wadada wawili walikuwa wanapigana kumgombea Mumeo (Baba Nang'oto). Ilikuwa vuta nikuvute na mumeo alikuwa kasimama tu anawaangalia akitabasamu. Baada ugomvi kwisha akaondoka na mmoja wao na kumwacha yule mwingine akitukana matusi kama ana akili nzuri.

Kisha nikaituma ile message

Baada ya dakika kama mbili hivi, akanipigia simu nami wala sikupokea simu yake... Akapiga tena na tena kama mara ishirini hivi wala sikupokea.

Akatuma message akiniuliza...

Hao wanawake unawajuwa, ...mume wangu na huyo mwanamke wameelekea wapi, wewe unawajuwa hao wanawake waliopigana, yaani hapa nimechanganyikiwa kwa kweli...!

Nikaisoma message yake wala sikuijibu, nikamchunia kimyaaa...!

Akanipigia tena simu mara tano, sikupokea simu zake, kimyaaa...! Akaniandikia message nyingine....

...Nakupigia jamani pokea simu basi nina pesa zako nataka nikupe... Naomba basi tukutane mjini unihadithie vizuri...!

Nami nikamjibu...

Nitumie hizo pesa kwenye Namba yangu ya Mpesa, ili nipitie sheli kujaza mafuta nije mjini kukupitia nikupeleke mahala walipo...!

Baada ya dakika 2 message ikaingia, kuangalia balance yangu ya Mpesa, nikakuta kaingiza pesa zangu zote ninazo mdai...!

Nikazima simu nikajilalia zangu kimyaaa.... Kama sio mie!

Wednesday, September 14, 2016

Daladala

Watu wengine bhanaa!!

Jana nilipanda daladala basi ile kaka yenu nikawa nimejiachia kuchati, kuna jamaa akawa anasoma msg zangu bila aibu yani anafutilia ninavyochati...

Basi nikasema ngoja nimtie Adabu.. Nikaamua nimtext jamaa "Oya Alex ngoja nilipue hii daladala muda ushafika" Yule jamaa akajirusha dirishani......
Na kavunjika miguu na kiuno........

Sipendi mambo ya kijinga mimi

Tuesday, September 13, 2016

Mwanamke

...ingekuwa vp dunia ingeongozwa na mwanamke kungekuwa hakuna vita, ungesikia tu.. Marekani aiongei na urusi, mara rwanda yainunia burundi, boko haramu yawapelekea umbea alshabaab, ethiopia yasusia misaada ya UN, mara djibout yamtuma balozi wake kuisuta sudan, waziri mkuu wa UK awachambe magaidi wa qt.. Yaani ingekuwa amani tu..!!
#shikamooni_wanawake

Friji

WABONGO KWELI MTIHANI
SINA HAMU NAO...!!

Jamaa alinunua friji jipya, akawaza namna ya kuondokana na lile la zamani, basi akaliweka nje ya nyumba yake na kuandika kibao:

"ANAYE TAKA KUCHUKUA, ACHUKUE BURE"

Watu wakawa wanapita wanafungua lakini kila mtu akawa anaogopa kuchukua maana hakuna aliyeamini mtu anaweza akagawa friji zima bure.

Baada ya kuona wiki imepita halijachukuliwa, akahamua kubadilisha kibao na kuandika:

FRIJI LINAUZWA SHILINGI LAKI MBILI NA NUSU TU

Usiku ule ule likaibwa

Sunday, September 11, 2016

Mkopo wa Chuo

Wenzako wanapokea mshahara M3 kila mwezi na bado wako single,wewe unapokea mkopo wa chuo unatuambia unataka kuoa....!!
Ulitakiwa upigwe KOFI la kichwa tu restore settings.
#PumbavuKabisa

Friday, September 9, 2016

STRESS NI NINI

Stress ni pale unapompa msichana lift halafu akazimia ndani ya gari yako na humjui wala hujui kwao. Ulimkuta tu njiani ukamsaidia.!

Noma zaidi ni pale unapoamua kumpeleka huyo msichana hospitali na akabainika ana mimba dokta akaanza kukupongeza kuwa unakaribia kuitwa baba!

Stress ya tatu ni pale unapokataa na kumwambia dokta mimba si ya kwako, mara ghafla msichana anazinduka na kudai mimba ni ya kwako?

Stress ya nne ni pale dokta anapoamua kukupima ili kuthibitisha, na baada ya vipimo anakwambia mimba si yako kwakuwa huna uwezo wa kumpa mwanamke mimba.!

Stress ya mwisho ni pale,, unaporidhika majibu ya doctor kuwa huna uwezo wa kumpa mwanamke mimba lakini unakumbuka nyumbani una mke na watoto wawili.....!!!!!!

Mtangazaji

Nimejisikia furaha sana leo nimewasha Redio nkasikia Mtangazaji wa KIKE  ananambia "MPENZI MSIKILIZAJI NAKUPENDA SANA ENDELEA KUWA NA MIMI KTK KIPINDI CHANGU"!!
Nimefurahi sana ila bado cjampa jibu kama na mimi nampenda au la!!

Demu

Umexhawah kuwa single had ukaamua kununua viatu vya kike kixha ukaviweka mlangon ili majiran wakipita wajue una demu ndani...

KUA SINGLE NAO NI UGONJWA EEENH

Mbuzi wa IDD

Family walinunua mbuzi wa IDD kabla kwa miezi miwilli.
Mbuzi akawazoea sana hio family na akawa anakula nao na kulala nao.
Siku ya IDD ilipokaribia mbuzi aliingia nyumbani huku machozi yanamtoka
Akaulizwa kwa nini unalia?
Akasema majirani wote wamenunua mbuzi wa IDD isipokuwa sisi.

Mhudumu

Leo nilienda kula hotelin nikamkuta ex wangu analumbana na wahudum kumbe kala kashindwa kulipa ikabidi wampeleke jikoni akasaidie kumenya viazi ili wamsamehe deni! Asee ilinigusa mnoo nikamwita yule mhudumu nikampa hela wanunue gunia jingine la viazi

Kang'atwa na nyoka

mdada:-    Bby naomba hela nimpeleke mdogo wangu hospital kang'atwa na nyoka
JAmaa:- embu mpe huyo nyoka simu niongee nae..
maisha yanakaba..

Hoteli

Kuna demU ameangusha kipochi leo, nikamwambia "Excuse me madam" akasema "I have a boyfriend" saa hii niko kwa hoteli nakula kuku••

#Maringo_sipendangi..

Salon

DADA alienda Salon wakati anasukwa akaingia MKAKA mtanashati, DADA akaamua kujaribu bahati yake.
DADA:Mambo?
KAKA:Poa.
DADA:Mimi na wewe tunaweza kuongea baade?
KAKA:Kuhusu nini?
DADA:Nimekupenda nataka nikutoe out.
KAKA:Sawa ila nitamwambia nini MKE wangu?
DADA:Aah ilo sio tatizo mdanganye tu,mwambie unakwenda kumtembelea rafiki yako hospitalini.
KAKA:Mwambie mwenyewe huyo hapo anayekusuka.Unajua nn kiliendelea?
Subiri ni chaji cm.

Thursday, September 8, 2016

Wanawake banaa..

Akikuta Pesa kwenye suruali wakati Wa kufua hata hasemii inaondoka kimya kimya   ..ila akute kondom sasa izo kelele zake utajuaa kama ulioa mwanamke au kipaza sauti
Kutoka mahali.

Mungu anawaona

Sunday, September 4, 2016

Panya

Nimeingia chumban  nikakuta panya wamekula dawa yangu ya menoo, Na mimi nimechukua yakwao nikanywa. Sipendagi ujinga mimi

Mwanafunzi

Unamtongoza mdada anakujibu et "bado nasoma" Dada kwani nimesema ukinikubalia ntakuchania Madaftari?

Tuesday, August 23, 2016

Chombo cha moto

Sheria inasema kila anaetembea na chombo cha moto barabarani sharti awe na lessen sasa lakini nashangaa wauza kahawa hawawakamati wakati wanatembea na vyombo vya moto barabarani

Sunday, August 7, 2016

My x

Et jana nmemtext *X* wangu *Hi*...et aka update status whatsapp yake                        "I am happy without you"                           
wakati mie nlitaka kumwambia tuu nmemwona baba ake mjini kavaa koti langu... I WANT IT BACK.

Saturday, July 9, 2016

Mwizi

Huku kwetu Mwizi Kapigwa Mpaka Wamemkata Mkono wasamaria Wema Wakamsaidia Kumpeleka Hospital Wakati Doctor Anamhudumia Akawa Ameenda Kuchukua Nyuzi Kurudi mwizi Hayupo Kaamsha na Simu Ya Doctor Na Mkono Kawaachia

Monday, May 16, 2016

Single

Eti ushawahi kuwa single hadi unajiuliza kwani ile mbavu yako ya kushoto iliyotolewa ilipikwa supu nin?!

Sex scene

Ushawahi kuwa nyumbani na wazazi mnaangalia movie halafu ghafla inatokea sex scene watu wanapigana mabusu wanarushana kitandani... Dingi anapagawa Ile kuua soo anakuuliza "Joshua? Ushapiga pasi GARI...!!!"
Nawe ulivyochanganyikiwa unajibu
"Umeme umekatika mzee..."

Saturday, May 14, 2016

Umezaliwa wapi?

Mtoto: Baba, kwani wee umezaliwa wapi?
Baba: Mbeya
Mtoto: na mama?
Baba: Tanga
Mtoto: na mimi?
Baba: Dar
Mtoto: sasa tumekutanaje?!

Sunday, April 17, 2016

Mmeo

Kuna Jamaa Kwenye Daladala Hapa Alikuwa Anaongea Na Simu....... Halooo Leo Sitaweza Kuja Nimepanda Gari Moja Na Mmeo...... Unaambiwa Wanaume Wote wenye Wake.... Wamemng'ang'ania Aoneshe Hiyo Namba Aliyokuwa Anaongea Nayo...... Sijui Kamalizana Nao Vipi Maana Mimi Nilishuka Kituo Kilichofuata.

Friday, April 8, 2016

Faraja

Ukikaa ukitafakari kuna milio mingi saana duniani ya gitaa,kinanda,pikipiki,gari etc.....lakini ule mlio m1 wakati ATM inatoa fedha ule grrrrr grrrr hua una faraja saana moyoni.... Daah pesa huyu

Wednesday, April 6, 2016

Unywaji pombe

Chukua tahadhari,

Unywaji pombe kupita kiasi hupelekea upungufu wa kumbukumbu na matatizo mengine mengine......... ambayo siyakumbuki vizuri!

Bahati iliyoje

BAHATI ILIOJE HII JAMANI.
××××××××××××××××××

Kuna siku nilikuwa maeneo ya Mjini kati
(City Center), nikaipenda suruali moja ya
shilingi 15,000/= na pesa sikuwa nayo
ikabidi niende kutoa kwenye ATM ya
Postal.
Nimefika pale sikukuta mtu hivyo
niliingia moja kwa moja, nimefika mle
ndani nikakuta Pesa Kibao zimemwagika
pale kwenye kitundu cha kutolea pesa,
ATM Card ilikuwepo pale imetokezea na
Pembeni kulikuwa na Pochi ya Kike
iliyoonekana kutuna vilivyo.
Kwa woga mimi huku nikitetemeka
mapigo ya moyo yakiwa yameongezeka
nikatizama nyuma yangu sikuona mtu,
nikachukua zile Pesa harakaharaka, ATM
na ile pochi.
Ile natoka nje kuna dada mmoja alikuwa
anakuja kwa kasi maeneo yale nikapata
uoga nikamuuliza "Samahani dada, kuna
kitu umesahau humu", yule dada
hakunijibu kitu kaingia kwenye chumba
cha ATM akachomeka Kadi kutoa hela
mi nikaondoka zangu fasta kuelekea
home.
Nimefika home nikajifungia ndani na
kuzibwaga zile pesa kitandani,
nikafungua wallet nikakuta imejaa
dollar, Vipodozi, iphone na ki-Nokia
kidogo cha tochi, ATM Card mbili za
Benki tofauti ambazo zilikuwa
zimezungushiwa karatasi iliyokuwa na
namba za siri za ATM zote, moyo
ukanilipuka paaaa!!! Nikaona bora
Nipumzike kwanza kitandani!!
Muda si mrefu ile iphone ikaanza kuita,
nilipoangalia halikutokea jina nikaona
bora nipokee nimsikilize anasemaje,
ilikuwa sauti ya kike iliyoongea kwa
huzuni kwa kubembeleza huku akilia na
alijitambulisha vizuri kuwa ile mali ni ya
kwake! Huruma ilinijia nikamwelekeza
nilipo aje kuchukua...
Hakuchukua muda akawa amefika nami
nikamkabidhi vitu vyote naye
akavihakiki na kukuta viko sana: Milioni
3 za Kibongo na Dollar 500. Dada
kanishukuru na kunipa ile Millioni 3 ya
kibongo mi nikazikataa kwasababu ni
mali yake na alizisahau tu.
Alinitoa hofu kwa kunisihi nichukue tu,
mi kama binadamu mwenyezi Mungu
atanilipa, nikakataa... Mwishowe
akaomba namba yangu na kuondoka
zake, akawa ameniacha ndani huku njaa
sasa nikaanza kuisikia, nilikuwa na buku
mbili nikaenda kula viepe kavu na soda
nikawa powa.
Sasa jana kanipigia simu kuwa anakuja
nimsubiri, dakika tano tu akanipigia tena
kuwa ameshafika yupo nje yupo ndani
ya Prado mpyaa nikaingia tukaondoka
akaenda kunionyesha kwake kisha
tukaelekea kwenye nyumba nyingine
iliyokuwa ndo imekamilika kujengwa
akaniambia hii itakuwa yako
akanikabidhi baadhi ya nyaraka na
funguo zote sikuamini...!!
Akanisindikiza kwangu, kufika home
ananiambia hiyo gari (Prado) nayo
ananiachia ni kwa mema tu
niliyomfanyia, ndani ya ile gari kulikuwa
na brifcase iliyokuwa na pesa
akaniambia pia hii pesa itakuwa yako ya
kuanzia maisha, na kumbe yule dada
alikuwa kanipenda akanikumbatia kwa
nguvu nikiwa pale kwenye seat oooh!!
umasikini baibai...
Akiwa kanikumbatia akihema kwa kasi
juu ya kifua changu. Mara nikahisi kubanwa na haja ndogo, nikakimbia fasta chooni na kuanza kukojoa, nasikia raaaha mkojo hauishi mara nikahisi mtu
akinishika begani na  kuniita kwa sauti.
"Anko ankoo we ankoo... amka unakojoa kitandaniii!!!".
"ALIKUWA MTOTO WA SISTA ALIKUWA
ANANIAMSHA !!"
Kumbe ndotooo mweeeh

Monday, April 4, 2016

Hali ya hewa

BOY: hellow baby

GIRL: Yes hubby

BOY: Unaona hali ya hewa kimvua kinashawishi...

GIRL: haswaaa tena kwa kilimo cha maharage....

Wednesday, March 30, 2016

Maisha yamenishinda

Jamaa kamkuta mwanamke mmoja pale Ferry analia,

JAMAA: Nini shida mama angu?

MDADA:Heri nife, maisha yamenishinda

MJAMAA: Huna haja ya kufa, sikiliza mimi ni baharia na meli yetu inaenda Ulaya leo, kama unataka ingia kwenye boksi nikakufiche stoo, meli ikitia nanga Ugiriki, nakutoa ukatafute maisha huko. Bibie akaona heri hilo akaingia kwenye boksi, jamaa akambeba na mdada akajikuta yuko kwenye stoo moja wapo katika meli, jamaa akawa anamletea chakula kila siku na mara nyingine yeye mwenyewe analala huko kwenye hako kastoo kama binadamu wengine walio kamilika walikuwa wanafanya na ya kwao huko huko kwahyo safari ilikuwa nzuri hasa kwa jamaa, kila mara akimhakikishia mdada kuwa wameshapita visiwa vya Komoro, siku nyingine akimwambia wako India. Zilipita wiki mbili ndipo yule mdada akagundulika na nahodha wa chombo hicho.

NAHODHA:We unafanya nini humu?

MDADA:Chonde naomba msinitupe baharini, nilindeni mkifika Ugiriki mnishushe

NAHODHA: Unajua mbona sikuelewi? Mdada akalazimika kumueleza nahodha ishu nzima.

NAHODHA:Dah wala usipate taabu sikutupi popote, ila jamaa yako kakudanganya hii si meli ya kwenda Ulaya ni pantoni ya kwenda Kigamboni, umekuwa unazunguka hapa hapa Dar siku zote hizo, haya tukifika Kigamboni  shuka...

My relationship

Kuna wakati WADADA naona hawako seriously.... Unakuta mtu anaomba Mungu daily mpaka kwenye status anaandika "GOD BLESS MY RELATIONSHIP "........wakat huo ana date na wanaume 11......🏻sasa si bora aseme God bless my TEAM

Kifo sio kizuri

Hizi mila zingine sio nzuri.......

Juzi nimeenda kuzika rafiki yangu huko kijijini kwao, sasa utaratibu ni kua baada ya kuzika mzee wa kimila hua anaamka na kutangaza atakayefata kufa mkiwa bado eneo la kaburi. Mzee huyo alipoamka akasema mtu wa kwanza kutoka eneo la kaburi ndio atakaefata kufa. Leo siku ya tatu bado tunazunguka zunguka tu hapa kaburini pamoja na yule mzee...kweli kifo sio kizuri...

Mwalimu

Mzee: Dereva ongeza sauti tumsikilize Mwalimu Nyerere!!

Dereva: ungemsikiliza mwalimu wako miaka iyo saivi ungekua na gari yako.

Sunday, March 20, 2016

Frank amefariki

Mume katoka mihangaikoni na kurudi nyumbani anamkuta Mke wake ana huzuni na majonzi huku macho yake Yakiwa yamevimba kwa kulia.

mume: Mbona una hali hiyo mamaa!?
Mke: Frank amefariki.

Kwa hali aliyomkuta nayo ikabidi amuache apumzike aakatoka zake na kwenda varandani kupata chakula.

Mume akaamua kumuuliza dada wa nyumbani.... na kujibiwa hajala amejifungia chumbani tokea aliporudi kazini...

Mume akabaki na mawazo tele juu ya Frank aliyefariki ni nani!!???? Akiangalia anamarafiki na ndugu wanaoitwa Frank. Akapiga moyo konde nakuingia kulala.

Asubuhi wakiwa mezani wanakunywa chai.

Mume: huo msiba ni wa Frank gani na unafanyikia wapi ili nipange ratiba zangu za leo.

Mke: Frank Xavier

Mume: ndio nani huyo mbona hilo jina sijawahi kulisikia?

Mke: si yule wa Kwenye ISIDINGO

Mume: ..*¤*.*¤.¤..¤.*

Saturday, March 19, 2016

Kitambulisho

MJINI SHULE!!
Chiz kaokota elf kumi jamaa mmoja aliekuwa anapita zake akamuona
JAMAA; oy samahan hicho ni kitambulisho changu!
CHIZI: Ww hata kama cna akil vzur hich xo kitambulisho ni ela ww
JAMAA: angalia vzur!
CHIZI: kama kwel n kitambulish chako w unaitwa nan?
JAMAA; benki kuu ya tanzania
CHIZI: ulizaliwa mwak gan?
JAMAA: mwaka 10000
CHIZI: dah kwel chako samahan kwa usumbuf
JAMAA: aina noma ukiviona vingine basi unitafute
CHIZI:poa

Friday, March 18, 2016

Mama mkwe

Mama mkwe kamkuta mkwe (mume wa bintiye) sebuleni akiwa kafura na kapandisha hasira anadai ataua mtu.

Mama Mkwe: Mwanangu kwani kuna nini jamani?
Jamaa: Leo namuua mwanao, mshenzi sana.
Mama Mkwe: Tulia jamani, kimetokea nini?
Jamaa: Mwanao mshenzi sana, nilikuwa nimesafiri, nikamtumia meseji kuwa nakuja, eti bado leo nimefika nimemkuta na mwanaume kwenye kitanda chetu, dharau gani hii, sikubali leo tunagawana majengo ya serikali, yeye anaenda kulala Muhimbili mi naenda kulala Segerea
Mama Mkwe: Subiri kwanza, mwanangu hayuko hivyo lazima kuna maelezo fulani kuhusu hili ngoja nimuulize...mama mkwe akamfwata mwanawe na baada ya muda akarudi sebuleni.
Mama Mkwe: Unaona, nilijua mimi lazima kuna sababu. Kumbe mwenzio hakupata ile meseji uliyomtumia.

Thursday, March 17, 2016

Mkulima

Mkulima Jipu......

MWANDISHI: Wewe unawalisha ng'ombe chakula gani?,
MKULIMA: Ng'ombe yupi Mweupe au Mwekundu?
MWANDISHI: Ng'ombe mweupe
MKULIMA: Ninamlisha nyasi na viguta vya mahindi,
MWANDISHI: Na mwekundu??
MKULIMA: vilevile nyasi na viguta vya mahindi,
MWANDISHI: ahaa sawa,na sehemu ya kulala ni wapi?
MKULIMA: Ng'ombe yupi mweupe au mwekundu?
MWANDISHI: Mweupeee!!!
MKULIMA: Mweupe ninamlaza bomani kulee,
MWANDISHI: na mwekundu?
MKULIMA: vilevile ninamlaza na mwenziwe!!!!
MWANDISHI: Hii sehemu yote majumba mengi, wakienda kulisha unafanyaje?
MKULIMA: Yupi mweupe au mwekundu?
MWANDISHI: Woteee!!!! {kwa hasira}
MKULIMA: Mweupe nina mfunga kamba na kumzungusha malishoni na kumrudisha,
MWANDISHI: na mwekundu vilevile?
MKULIMA: Mwekundu?, mwekundu ninamfunga
kamba na kuzunguka nae kama mwenziwe!!!
MWANDISHI: Kwanini kila mara nikikuuliza huduma za ng'ombe zako unaniuliza mweupe
au mwekundu halafu inatokea kuwa kazi zao wote ni sawa??,
MKULIMA: Kwasababu Ng'ombe mweupe ni wangu,
MWANDISHI: Na mwekundu?
MKULIMA: Ni wangu vilevile!!!!!

Wednesday, March 16, 2016

Kazi

WAKUU WA MIKOA wamepewa siku 15 tu wahakikishe hakuna vijana watakao kaa bila kazi.

Kama kijana huna kazi unawekwa ndani.. ukitoka unajikuta huna kazi unarudishwa tena ndani..

Ukitoka unakuta masharti ya kazi uwe hujawahi kufungwa jela. . Unakosa hio kazi alafu unarudishwa tena ndani.🤓🤓

Tuesday, March 15, 2016

Book-keeping

Katika pitapita za JAMBAZI ucku
Alisikia watu wakibishana
kuhusu MILIONI 50,
mmoja
anasema ziweke kwa Nathan
Mwingine akasema tuweke
Bank.
Jambaz kusikia hivyo akaamua kuvunja
mlango,
Ile
kuingia akakuta wanafunzi
wana solve Book-keeping..

Utatembea

Jana nilikuwa kwenye mkesha kanisani, wakati tupo kwenye maombi, jirani yangu akanigusa begani nilipojeuka akaniambia amini leo hii utatembea. Nikashangaa nakujiuliza kimoyomoyo nitatembea, Kivipi wakati sina ulemavu wowote au tatizo la kunifanya nishindwe kutembea!
Nikaona isiwe tabu nikamjibu tu 'AMEEEN'
Baada ya mkesha nimefika kituoni nipande gari la kuelekea nyumbani kujicheki nikakuta nimeibiwa nauli.
Basi ......

Monday, March 14, 2016

My relationship

Kuna wakati WADADA naona hawako seriously.... Unakuta mtu anaomba Mungu daily mpaka kwenye status anaandika "GOD BLESS MY RELATIONSHIP "........wakat huo ana date na wanaume 11......🏻sasa si bora aseme God bless my TEAM

Kuvuta bangi peke yako

Ushawai vuta bangi pekeako kwa room, ukaamua kupiga nguo zako zote pasi.. Halafu ukimaliza unagundua hukuwa umewasha socket?

Mbezi ya Kimara

Yaani nimepanda gari ya mbezi ya kimara hapa ubungo (mawasiliano) nikijua ni gari ya mnazi mmoja, nimekuja kushituka kusikiaa kimara mwisho.

Tatizo haya magari makubwa ubavuni yana ruti zaidi ya sita.

Ila nafurahi nimepotea kwenye basi, ningekuwa nimepotea kwenye pantoni si ningekuwa kwenye boti za pemba sasa.

Au kwenye treni badaya ya ile ya ubungo sasa ningekuwa nakaribia zambia.

Sunday, March 13, 2016

Maisha yamenishinda

Jamaa kamkuta mwanamke mmoja pale Ferry analia,

JAMAA: Nini shida mama angu?

MDADA:Heri nife, maisha yamenishinda

MJAMAA: Huna haja ya kufa, sikiliza mimi ni baharia na meli yetu inaenda Ulaya leo, kama unataka ingia kwenye boksi nikakufiche stoo, meli ikitia nanga Ugiriki, nakutoa ukatafute maisha huko. Bibie akaona heri hilo akaingia kwenye boksi, jamaa akambeba na mdada akajikuta yuko kwenye stoo moja wapo katika meli, jamaa akawa anamletea chakula kila siku na mara nyingine yeye mwenyewe analala huko kwenye hako kastoo kama binadamu wengine walio kamilika walikuwa wanafanya na ya kwao huko huko kwahyo safari ilikuwa nzuri hasa kwa jamaa, kila mara akimhakikishia mdada kuwa wameshapita visiwa vya Komoro, siku nyingine akimwambia wako India. Zilipita wiki mbili ndipo yule mdada akagundulika na nahodha wa chombo hicho.

NAHODHA:We unafanya nini humu?

MDADA:Chonde naomba msinitupe baharini, nilindeni mkifika Ugiriki mnishushe

NAHODHA: Unajua mbona sikuelewi? Mdada akalazimika kumueleza nahodha ishu nzima.

NAHODHA:Dah wala usipate taabu sikutupi popote, ila jamaa yako kakudanganya hii si meli ya kwenda Ulaya ni pantoni ya kwenda Kigamboni, umekuwa unazunguka hapa hapa Dar siku zote hizo, haya tukifika Kigamboni  shuka...

Friday, March 4, 2016

Anapenda Hela

Ushawahi kuwa na demu anapenda hela mpaka unamtumia vocha anakuuliza "baby ya kutolea je ?"

Wednesday, March 2, 2016

Machizi

chizi wawili walipanda train wakienda mombasa
chizi 1:'unaona miti vile inakimbia '
chizi 2:'eee itabidi tupande miti tukirudi'.

Sunday, February 14, 2016

Mwanamke

Wakati Tarime mwanamke anamnyang'anya Jambazi bunduki.....! Dar mwanamke anamkimbia mende!

Friday, February 12, 2016

Mke wangu

Jamaa kapiga simu kumuuliza sheikh.
Jamaa: Sheikh kila siku usiku nikishtuka kwenye usingizi naona nuru/mwanga inatoka kwenye uso wa mke wangu na yeye kajifunika blanket. Na nakuwa nakhofu kukamilisha usingizi wangu. Jee hii ni dalili ya kuwa mke wangu miongoni wa watu wema??

Sheikh: badilisha pin code yako ya simu maana mke wako anapekuwa simu yako wakati umelala

Thursday, February 11, 2016

Usikate miti

Je wajua???
Binadamu ndio kiumbe pekee awezaye kukata miti akatengeneza karatasi kisha juu ya karatasi akaandika "USIKATE MITI"

Sunday, February 7, 2016

Ubuyu

MUME: Vipi wife, leo utaratibu wa kuchagua nini kipikwe si unaendelea?

MKE: Kama kawaida mume wangu, ila leo majanga.

MUME: Kuna nini tena?

MKE: Juzi we si ulichagua pilau tukapika? Na jana mimi nikachagua mtori ukapikwa?

MUME: Ndiyo mke wangu.

MKE: Sasa leo zamu ya mwanao Junior., na ameshachagua hatuna budi kutii..

MUME: Kachagua nini?

MKE: Ubuyu!!

Friday, January 29, 2016

Madevu

Jamaa akiwa nyumba ndogo karelax na Mdada, Mdada kwa sauti laini akaanza;
MDADA: Jamani lini utanyoa hizo ndevu, mi sizipendi
SOUD: Bwana ziache mke wangu anazipenda sana hatutaelewana nikizinyoa!
MDADA: Nyoa jamani, au hunipendi?
SOUD: Nakupenda, lakini kwa nini huzipendi?
MDADA: Unajua we handsome boy sana mpenzi, mi nataka niwe nauona uso wako wote swiry…
Soud hatimae akanyoa ndevu zote. Baadae akarudi nyumbani usiku akinyata taratibu na kufanikiwa kupanda kitandani wakati anaanza kulala tu. Mke wake akiwa usingizini akageuka na kumgusa mashavu,
MKE: We JULIUS, huogopi kufa, mume wangu atarudi muda wowote, ondoka haraka bwana!sije ukanivunjia ndoa yangu.....

Friday, January 22, 2016

Nimewaza tu

Nimekaaa nikawaza tu embu ngoja nisaidieni jamani..

Kama uko kwenye mapenzi na mtu zaidi ya mmoja na unasema wote unawapenda basi huo sio moyo tena ni memory card...

Japo kuna watu wana hard disk kabisa

Kuoa ni majaliwa

Kuna vitu ukiona kijana wakiume anavifanya Gheto ujue kuoa ni majaliwa
1.anapika chapati za kusukuma Gheto
2.Anakuna nazi Gheto
3.Anapika makande gheto
4.Ameweka midori kitandani
5.Ameweka kadi mezani
6.Ananunua gunia la mkaa anaweka gheto....
7. kaweka dressing table
8. kanunua vyombo vya ndani vya kutosha.
9. ananunua viungo vingi sana sokoni
10. anapenda kulakula hovyo

Hayo ni mambo yanayo bainisha kuwa upatikanaji wa mke kwa upande wake ni mdogo

Tuesday, January 19, 2016

Magonjwa

Teacher :: Tuandike aina ya magonjwa mbali mbali
Paul::H.I.V
Eliud: cholera
Chrispin: malaria...
Deborah: typhoid
Edson: /

Teacher: Sasa wewe Edson ndo ugonjwa gani huo umeandika  /?
Edson: stroke

Kazi za wazazi

Mwalimu kauliza swali darasani
wanafunzi wataje
kazi za wazazi wao:
TINA: mimi baba yangu
mfanyabiashara mama
yangu mwalimu.
MWALIMU: Safi, haya juma
JUMA: Baba yangu dereva mama
yangu hafanyi
kazi.
MWALIMU: Vizuri, haya Zogo.
ZOGO: Mimi mama yangu malaya
anajiuza baba
simjui.
MWALIMU: Pumbavu wewe, nenda
ofisini kwa
mwalimu mkuu ukamueleze upuuzi
wote
uliosema hapa. Zogo anaenda ofisini
anarudi
huku anatabasamu na anakula
biskuti.
MWALIMU: Mwalimu mkuu kakupa
adhabu gani?
ZOGO: Kaniambia nimpe namba ya
mama...

Saturday, January 16, 2016

Kuoa ni majaliwa

Kuna vitu ukiona kijana wakiume anavifanya Gheto ujue kuoa ni majaliwa
1.anapika chapati za kusukuma Gheto
2.Anakuna nazi Gheto
3.Anapika makande gheto
4.Ameweka midori kitandani
5.Ameweka kadi mezani
6.Ananunua gunia la mkaa anaweka gheto....
7. kaweka dressing table
8. kanunua vyombo vya ndani vya kutosha.
9. ananunua viungo vingi sana sokoni
10. anapenda kulakula hovyo

Hayo ni mambo yanayo bainisha kuwa upatikanaji wa mke kwa upande wake ni mdogo

Friday, January 15, 2016

Nyumba inauzwa

Kuna nyumba inauzwa  milioni mbili ipo ndani ya fensi ya matofali inaeneo lenye 40m x 35m inavyumba nane, na sehemu ya kupaki gari, ina maji na umeme.  Ipo mita 100 kutoka barabarani ina x lakini inafutika.

Tuesday, January 12, 2016

Zimwi

RIWAYA YA MAANDISHI:

Mheshimiwa mmoja baada ya kupata cheo akapewa nyumba mitaa ya watu wenye pesa. Akahamia huko akiwa na mke na mwanae. Siku moja mwanae aliyekuwa kazoea maisha ya Uswazi akawa anawinda ndege na manati kwenye uwanja wa jumba lao, bahati mbaya jiwe likapitiliza na kwenda kuvunja kioo cha nyumba ya jirani.

Mheshimiwa na mkewe wakaamua kumfuata mwenye nyumba wakamuombe msamaha. Walipogonga mlango akafungua mbaba mmoja akawakaribisha kwa heshima, wakaingia na kuanza kujieleza. 'Samahani sisi tumehamia karibuni hapo nyumba ya pili, mwanetu kavunja kioo chako kwa bahati mbaya, tumekuja kuomba msamaha na kuona kama tunaweza kutengeneza'.

Mwenyeji wao akawaomba wakae kisha akawaambia, 'Naomba niwahadithie kitu. Kwanza mimi nawashukuru nyinyi na mtoto wenu. Mwenye nyumba hii ni mchawi mkubwa sana, mimi ni ZIMWI alikuwa amenifungia kwa zaidi ya miaka 20 kwenye kichupa ambacho kilikuwa kwenye dirisha lililovunjwa. Baada ya dirisha kuvunjika na chupa nacho kikavunjika nami nimekuwa huru. Kwa hiyo kwa shukurani ombeni chochote mtakacho nitawapa, nina uwezo huo'

Hapo hapo muheshimiwa akauliza tena,'Yaani kitu chochote?' Akajibiwa 'Ndio'. Basi pale pale akasema, ' Mimi naomba bosi wangu asinifuatilie na madhambi yangu ofisini yasahaulike kabisa na pia niwe bilionea mpaka nife' Akajibiwa ,' Hilo jambo dogo sana kwangu, hakufuati tena na kesho utaamka tajiri. Mama nae akaomba vyake, 'Mi nataka niwe na nyumba kila nchi duniani na niwe na biashara Dubai na China na Hong Kong' Akajibiwa, 'Umepata mama, kuanzia kesho hayo ni yako.

ZIMWI likasema "Mimi nawashukuru kwa uhuru wangu lakini nina kaombi kadogo".  Mheshimiwa haraka akajibu, 'Sema tu wewe ni kama ndugu yetu sasa' Basi ZIMWI likasema, 'Naomba mkeo abaki hapa kama masaa mawili tu, unajua kifungo nilichofungwa kilinizuia kila kitu, hata mke sijapata kipindi chote hicho. Nikimaliza tu hilo nitaondoka kurudi kwetu Uzimwini hamtaniona tena, itakuwa siri yetu'.

Mme na mke wakajadiliana wakaona utajiri waliopata ni mkubwa sana, na hilo jambo ni dogo sana la mara moja tu tena kwa siri, wakakubali sharti. Mke akabaki pale kwa masaa kadhaa. Shughuli ilipokwisha, mama wa watu akiwa anajitayarisha kurudi kwa mumewe kichwani akiwaza utajiri, ZIMWI likakohoa kidogo na kumuuliza yule mama, 'Samahani una miaka mingapi na mumeo ana miaka mingapi?" Mama wa watu akajibu, 'Mie nina miaka 40 mume wangu ana miaka 46' Yule mbaba Zimwi akacheka sanaa, na kusema "Sasa nyinyi wakubwa wazima mpaka leo mnaamini stori za  MAZIMWI?

Ukoo wao

Mtoto wa miaka sita alimuuliza babake:
MTOTO: Baba, eti sisi wanadamu tulikuja vipi duniani ?
BABA: Mungu alimuumba Nabii Adam na Hawa. Kisha wao wakaanza kuzaa watoto na watoto wakazaa mpaka tukazaliwa sisi. (Mtoto hakuridhika akamfuta mamake)
MTOTO: Mma, eti sisi wanadamu tulikuja vipi duniani?
MAMA: Wanasayansi wamesema sisi tulitokana na Manyani baadae tukawa Binadamu. (Mtoto akarudi kwa baba)
MTOTO: Baa mbona mama ansema sisi tulikuwa Manyani mwanzo? Au wanidanganya?
BABA: Mwanangu, mimi nimekuelezea kuhusu ukoo wetu. Mamako amekuelezea kuhusu ukoo wao.

Familia za watu

Ati john is 10 years older than his father, his mother is 40 years old.,20 years younger than john.,find the Age of
1.john
2.father
3.mother

Hii swali nilikuwa naruka..Sio ati ujinga...ni vile tu sipendi kuingilia mambo ya familia za watu..

Kande na Parachichi

Unaenda hotelini unaona menu imeandikwa:
Sauteed white corn, rare lucy beans, garnished with rift potatoes & topped with organic unprocessed guacamole.

Price: TSH 44,000

Unaagiza! Ukiletewa ndio unagundua kwamba: Ni Kande  na parachichi.....

Monday, January 11, 2016

Inside the bank

Jost goes on the ATM and withdraw all the money from the ATM.

Then he goes inside the same bank and deposit all the money he withdrew from the ATM, telling the Teller, "my money is not safe outside in the ATM. People are just withdrawing anyhow and they might end up withdrawing what is mine. Keep my money inside the bank please."

Monday, January 4, 2016

English lesson

During an English lesson, the teacher instructed his students to write a composition.

QN: Assume you are in a war, write a story?

One student did not write any thing & kept seated. The Teacher got puzzled, walked to the student's desk & asked him why he was not doing the exercise.

The student replied,  "I was killed immediately at the beginning of the war".