tangazo one

tangazo one

Abidal

Abidal

karibuni

ni mara chache sana tunapata muda wa kujiuliza juu ya umuhimu wa watu waliotuzunguka, na maisha yetu yangekuwaje bila wao? wape nafasi na usisite kuwaambia jinsi unavyojisikia juu yao na umuhimu wao kwako. ASANTE KWA KUWA SEHEMU YA MAISHA YANGU.

Thursday, May 22, 2014

Padre na Mbunge

Padre mmoja mzee alistaafu na wanaparokia walimfanyia sherehe kubwa. Katikasherehe hiyo, mbunge wa eneo hilo alipangwa kutoa hotuba ya shukurani yakumuaga padri huyo kwa niaba ya wanaparokia wote. Bahati mbaya, mbungealichelewa kufika ....
Mc akamwomba padri aseme machache wakati wanamsubiri mheshimiwa mbunge.
Padri hakujipanga kusema kitu lakini kwa kujitahidi, aliongea.
"Wapendwa, naikumbuka sana siku nilipofika katika kanisa hili kwa mara yakwanza, ila nilipata mshangao siku nilipoanza kuungamisha. Mtu wa kwanzakabisa kumuungamisha alinishangaza sana. kwani alisema amemwibia bosi wakeTV, amemwibia ndugu yake pesa za urithi, amezini na jirani yake, na piakatembea na house girl wake. Nikapata picha kuwa kumbe watu wa kanisa hilindivyo walivyo, nikasikitika sana. Kumbe nilifikiria tofauti. Kwani baadayenikakuta kumbe watu wa hapa ni wazuri sana na hawatendi dhambi mara kwa marana ni wastaarabu sana".

Mara mheshimiwa mbunge akawasili, padri akakatisha maongezi na mbungeakaanza kuhutubia. "Ndugu wapendwa, naomba mniwie radhi kwa kuchelewa kwaninilikuwa na majukumu makubwa ya kiserikali. Pia ninayo furaha kubwa kwakunipa nafasi hii kuhutubia kwa niaba yenu. Mimi nina bahati sana kwani padri huyu alipokuja hapa, mimi nilikuwa mtu wa kwanza kwenda na kuungama kwake....